Kum. 25:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Washindanapo waume wao kwa wao, akakaribia mke wa mmojawapo, ili kumwokoa mumewe katika mkono wa ampigaye, yule mke akatoa mkono wake, na kumkamata tupu yake;

12. umkate ule mkono wake, lisiwe na huruma jicho lako.

13. Usiwe na mawe ya kupimia mbalimbali, kubwa na dogo, katika mfuko wako.

14. Usiwe na vipimo mbalimbali, kikubwa na kidogo, katika nyumba yako.

15. Uwe na jiwe timilifu la haki, uwe na kipimo kitimilifu cha haki; zipate kuwa nyingi siku zako, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako.

16. Kwa kuwa wote wayatendao mambo kama haya, wote watendao yasiyo haki, ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako.

Kum. 25