Isa. 57:19-21 Swahili Union Version (SUV)

19. Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema BWANA; nami nitamponya.

20. Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka.

21. Hapana amani kwa wabaya; asema Mungu wangu.

Isa. 57