Isa. 43:17-22 Swahili Union Version (SUV)

17. atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi.

18. Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.

19. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.

20. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu;

21. watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.

22. Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli.

Isa. 43