17. atoaye gari na farasi, jeshi la askari na uwezo; wamelala, hawataondoka; wametoweka, wamezimwa mfano wa utambi.
18. Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.
20. Wanyama wa kondeni wataniheshimu, mbweha pia na mbuni; kwa sababu nimewapa maji jangwani, na mito nyikani, ili kuwanywesha watu wangu, wateule wangu;
21. watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.
22. Lakini hukuniita, Ee Yakobo, bali umechoka nami, Ee Israeli.