Isa. 40:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye,Itengenezeni nyikani njia ya BWANA;Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu.

4. Kila bonde litainuliwa,Na kila mlima na kilima kitashushwa;Palipopotoka patakuwa pamenyoka,Na palipoparuza patasawazishwa;

5. Na utukufu wa BWANA utafunuliwa,Na wote wenye mwili watauona pamoja;Kwa kuwa kinywa cha BWANA kimenena haya.

6. Sikiliza, ni sauti ya mtu asemaye, Lia!Nikasema,Nilie nini? Wote wenye mwili ni majani,Na wema wake wote ni kama ua la kondeni;

Isa. 40