1. Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.
2. Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.
3. Tena macho yao waonao hayatakuwa na kiwi, na masikio yao wasikiao yatasikiliza.
4. Tena moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu maarifa, na ndimi zao wenye kigugumizi zitakuwa tayari kunena sawasawa.
5. Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala ayari hatasemwa kwamba ni karimu.
6. Maana mpumbavu atanena yaliyo upumbavu, na moyo wake utafanya maovu, ili kutenda hila na kusema yasiyo kweli juu ya BWANA, ili kuziacha nafsi za watu wenye njaa hazina kitu, na kukikomesha kinywaji chake mwenye kiu.