5. BWANA amelivunja gongo la wabaya,Fimbo ya enzi yao wenye kutawala.
6. Yeye aliyewapiga mataifa kwa ghadhabu,Kwa mapigo yasiyokoma;Aliyewatawala mataifa kwa hasira,Ameadhibiwa asizuie mtu.
7. Dunia yote inastarehe na kutulia;Hata huanzilisha kuimba.
8. Naam, misunobari inakufurahia,Na mierezi ya Lebanoni, ikisema,Tokea wakati ulipolazwa chini wewe,Hapana mkata miti aliyetujia.
9. Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako,Ili kukulaki utakapokuja;Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako,Naam, walio wakuu wote wa dunia;Huwainua wafalme wote wa mataifa,Watoke katika viti vyao vya enzi.
10. Hao wote watajibu na kukuambia,Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi!Wewe nawe umekuwa kama sisi!
11. Fahari yako imeshushwa hata kuzimu,Na sauti ya vinanda vyako;Funza wametandazwa chini yako,Na vidudu vinakufunika.
12. Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!Jinsi ulivyokatwa kabisa,Ewe uliyewaangusha mataifa!
13. Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni,Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu;Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,Katika pande za mwisho za kaskazini.
14. Nitapaa kupita vimo vya mawingu,Nitafanana na yeye Aliye juu.
15. Lakini utashushwa mpaka kuzimu;Mpaka pande za mwisho za shimo.
16. Wao wakuonao watakukazia macho,Watakuangalia sana, wakisema,Je! Huyu ndiye aliyeitetemesha dunia,Huyu ndiye aliyetikisa falme;
17. Aliyeufanya ulimwengu ukiwa, akaipindua miji yake;Asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?
18. Wafalme wote wa mataifa wamezikwa wote kwa heshima,Kila mmoja ndani ya nyumba yake mwenyewe;