10. Hao wote watajibu na kukuambia,Je! Wewe nawe umekuwa dhaifu kama sisi!Wewe nawe umekuwa kama sisi!
11. Fahari yako imeshushwa hata kuzimu,Na sauti ya vinanda vyako;Funza wametandazwa chini yako,Na vidudu vinakufunika.
12. Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi!Jinsi ulivyokatwa kabisa,Ewe uliyewaangusha mataifa!
13. Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni,Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za Mungu;Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano,Katika pande za mwisho za kaskazini.