7. Wakasafiri kutoka Ethamu, na kurudi nyuma hata Pi-hahirothi palipokabili Baal-sefoni; wakapanga mbele ya Migdoli.
8. Wakasafiri kutoka hapo mbele ya Hahirothi, wakapita katikati ya bahari na kuingia jangwani; kisha wakaenda safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu, wakapanga Mara.
9. Wakasafiri kutoka Mara, wakafikilia Elimu; huko Elimu palikuwa na chemchemi za maji kumi na mbili, na mitende sabini; nao wakapanga hapo.
10. Wakasafiri kutoka Elimu wakapanga karibu na Bahari ya Shamu.
11. Wakasafiri kutoka Bahari ya Shamu, wakapanga katika nyika ya Sini.
12. Wakasafiri kutoka nyika ya Sini, wakapanga Dofka.
13. Wakasafiri kutoka Dofka, wakapanga Alushi.
14. Wakasafiri kutoka Alushi, wakapanga Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya watu kunywa.
15. Wakasafiri kutoka Refidimu, wakapanga katika nyika ya Sinai.
16. Wakasafiri kutoka nyika ya Sinai, wakapanga Kibroth-hataava.
17. Wakasafiri kutoka Kibroth-hataava, wakapanga Haserothi.
18. Wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga Rithma.
19. Wakasafiri kutoka Rithma, wakapanga Rimon-peresi.
20. Wakasafiri kutoka Rimon-peresi, wakapanga Libna.
21. Wakasafiri kutoka Libna, wakapanga Risa.
22. Wakasafiri kutoka Risa, wakapanga Keheletha.
23. Wakasafiri kutoka Keheletha, wakapanga katika mlima wa Sheferi
24. Wakasafiri kutoka huo mlima wa Sheferi, wakapanga Harada.
25. Wakasafiri kutoka Harada, wakapanga Makelothi.
26. Wakasafiri kutoka Makelothi, wakapanga Tahathi.