5. Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi, wakapanga katika Sukothi.
6. Kisha wakasafiri kutoka Sukothi, wakapanga Ethamu, palipo katika mwisho wa nyika.
7. Wakasafiri kutoka Ethamu, na kurudi nyuma hata Pi-hahirothi palipokabili Baal-sefoni; wakapanga mbele ya Migdoli.
8. Wakasafiri kutoka hapo mbele ya Hahirothi, wakapita katikati ya bahari na kuingia jangwani; kisha wakaenda safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu, wakapanga Mara.
9. Wakasafiri kutoka Mara, wakafikilia Elimu; huko Elimu palikuwa na chemchemi za maji kumi na mbili, na mitende sabini; nao wakapanga hapo.
10. Wakasafiri kutoka Elimu wakapanga karibu na Bahari ya Shamu.
11. Wakasafiri kutoka Bahari ya Shamu, wakapanga katika nyika ya Sini.
12. Wakasafiri kutoka nyika ya Sini, wakapanga Dofka.
13. Wakasafiri kutoka Dofka, wakapanga Alushi.
14. Wakasafiri kutoka Alushi, wakapanga Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya watu kunywa.
15. Wakasafiri kutoka Refidimu, wakapanga katika nyika ya Sinai.
16. Wakasafiri kutoka nyika ya Sinai, wakapanga Kibroth-hataava.
17. Wakasafiri kutoka Kibroth-hataava, wakapanga Haserothi.
18. Wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga Rithma.