23. Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo,Wala hapana uganga juu ya Israeli.Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa,Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!
24. Tazama, watu hawa wanaondoka kama simba mke,Na kama simba anajiinua nafsi yake,Hatalala hata atakapokula mawindo,Na kunywa damu yao waliouawa.
25. Balaki akamwambia Balaamu, Basi usiwalaani kabisa, wala usiwabariki kabisa.