Hes. 15:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,

2. Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtakapoingia nchi yenu ya kukaa, niwapayo,

3. nanyi mwataka kumsongezea BWANA sadaka kwa moto, kwamba ni sadaka ya kuteketezwa, au dhabihu ya kuchinjwa, ili kuondoa nadhiri, au kuwa sadaka ya hiari, au katika sikukuu zenu zilizoamriwa, ili kumfanyia BWANA harufu ipendezayo, katika ng’ombe, au katika kondoo;

Hes. 15