Hes. 12:6-11 Swahili Union Version (SUV)

6. Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.

7. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa;Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

8. Kwake nitanena mdomo kwa mdomo,Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo;Na umbo la BWANA yeye ataliona.Mbona basi ninyi hamkuogopaKumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

9. Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake.

10. Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.

11. Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.

Hes. 12