Hes. 12:5-9 Swahili Union Version (SUV)

5. BWANA akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.

6. Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.

7. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa;Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

8. Kwake nitanena mdomo kwa mdomo,Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo;Na umbo la BWANA yeye ataliona.Mbona basi ninyi hamkuogopaKumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

9. Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake.

Hes. 12