23. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
24. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
25. Kisha beramu ya marago ya wana wa Dani, ambayo yalikuwa ni nyuma ya marago yote, ikasafiri, kwa majeshi yao; na juu ya jeshi lake ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani;