Hes. 10:15-26 Swahili Union Version (SUV)

15. Na juu ya jeshi la kabila ya wana wa Isakari alikuwa Nethaneli mwana wa Suari.

16. Na juu ya jeshi la kabila ya wana wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.

17. Na maskani ilishushwa; na wana wa Gershoni, na wana wa Merari, walioichukua maskani, wakasafiri kwenda mbele.

18. Kisha beramu ya marago ya Reubeni ikasafiri kwenda mbele kwa majeshi yao; na juu ya jeshi lake alikuwa Elisuri mwana wa Shedeuri.

19. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Suri-shadai.

20. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.

21. Ndipo wakasafiri Wakohathi wenye kuvichukua vile vitu vitakatifu; na hao wengine wakaisimamisha maskani kabla hawajaja wao.

22. Kisha beramu ya marago ya wana wa Efraimu ikasafiri kwenda mbele kwa majeshi yao; na juu ya jeshi lake ni Elishama mwana wa Amihudi.

23. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.

24. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.

25. Kisha beramu ya marago ya wana wa Dani, ambayo yalikuwa ni nyuma ya marago yote, ikasafiri, kwa majeshi yao; na juu ya jeshi lake ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.

26. Tena juu ya jeshi la kabila ya wana wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani;

Hes. 10