Eze. 6:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Neno la BWANA likanijia, kusema,

2. Mwanadamu, uelekeze uso wako uitazame milima ya Israeli, ukaitabirie,

3. ukisema, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi milima na vilima, na vijito na mabonde; Tazama, mimi, naam, mimi, nitaleta upanga juu yenu, nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka,

4. Na madhabahu zenu zitakuwa ukiwa, na sanamu zenu za jua zitavunjika; nami nitawatupa wana wenu waliouawa mbele ya vinyago vyenu.

Eze. 6