1. Kisha akanileta mpaka langoni, yaani, lango lile lielekealo upande wa mashariki;
2. na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea kwa njia ya mashariki; na sauti yake ilikuwa kama mshindo wa maji mengi, nayo nchi iling’aa kwa utukufu wake.