Ayu. 8:13-18 Swahili Union Version (SUV)

13. Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu;Na matumaini yake huyo mbaya huangamia;

14. Uthabiti wake utavunjika,Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.

15. Ataitegemea nyumba yake, isisimame;Atashikamana nayo, isidumu.

16. Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua,Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.

17. Mizizi yake huzonga-zonga chuguu,Huangalia mahali penye mawe.

18. Lakini, aking’olewa mahali pake,Ndipo patamkana, na kusema, Mimi sikukuona.

Ayu. 8