20. Upate kuipeleka hata mpaka wake,Upate kuelewa na mapito ya kuiendea nyumba yake?
21. Hukosi unajua, maana ulizaliwa wakati huo,Na hesabu ya siku zako ni kubwa!
22. Je! Umeziingia ghala za theluji,Au umeziona ghala za mvua ya mawe,
23. Nilizoziweka akiba kwa wakati wa misiba,Kwa siku ya mapigano na vita?
24. Je! Nuru hutengwa kwa njia gani,Au upepo wa mashariki hutawanywaje juu ya nchi?
25. Ni nani aliyepasua mfereji kwa maji ya gharika,Au njia kwa umeme wa radi;