8. Hao vijana waliniona wakajificha,Nao wazee wakaniondokea na kusimama;
9. Wakuu wakanyamaa wasinene,Na kuweka mikono yao vinywani mwao;
10. Sauti yao masheki ilinyamaa,Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao.
11. Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia;Na jicho liliponiona, likanishuhudia.
12. Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia;Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.