Ayu. 29:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Hao vijana waliniona wakajificha,Nao wazee wakaniondokea na kusimama;

9. Wakuu wakanyamaa wasinene,Na kuweka mikono yao vinywani mwao;

10. Sauti yao masheki ilinyamaa,Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao.

11. Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia;Na jicho liliponiona, likanishuhudia.

12. Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia;Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.

Ayu. 29