Ayu. 29:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani,Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;

4. Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa,Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu;

5. Wakati Mwenyezi alipokuwa akali pamoja nami,Nao watoto wangu walipokuwa wakinizunguka;

6. Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi,Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta!

Ayu. 29