21. Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja,Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu.
22. Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu;Matamko yangu yakadondoka juu yao.
23. Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua;Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika.
24. Walipokata tamaa nikacheka nao;Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha.
25. Niliwachagulia njia, nikakaa kama mkuu wao.Nikakaa kama mfalme katika jeshi la askari,Mfano wa awafarijiye hao waombolezao.