Ayu. 29:21-25 Swahili Union Version (SUV)

21. Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja,Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu.

22. Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu;Matamko yangu yakadondoka juu yao.

23. Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua;Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika.

24. Walipokata tamaa nikacheka nao;Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha.

25. Niliwachagulia njia, nikakaa kama mkuu wao.Nikakaa kama mfalme katika jeshi la askari,Mfano wa awafarijiye hao waombolezao.

Ayu. 29