Ayu. 29:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,

2. Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya kale,Kama katika siku hizo Mungu aliponilinda;

3. Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani,Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;

4. Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa,Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu;

5. Wakati Mwenyezi alipokuwa akali pamoja nami,Nao watoto wangu walipokuwa wakinizunguka;

6. Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi,Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta!

7. Wakati nilipotoka kwenda mjini, hata langoni,Nilipokitengeza kiti changu katika njia kuu,

Ayu. 29