9. Je! Mungu atakisikia kilio chake,Taabu zitakapomfikilia?
10. Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi,Na kumlingana Mungu nyakati zote?
11. Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu;Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.
12. Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe;Mbona basi mmebatilika kabisa?
13. Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu,Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.
14. Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga;Na wazao wake hawatashiba chakula.
15. Hao watakaosalia kwake watazikwa katika kufa,Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.
16. Ajapokusanya fedha kama mavumbi,Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;