Ayu. 27:9-16 Swahili Union Version (SUV)

9. Je! Mungu atakisikia kilio chake,Taabu zitakapomfikilia?

10. Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi,Na kumlingana Mungu nyakati zote?

11. Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu;Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.

12. Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe;Mbona basi mmebatilika kabisa?

13. Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu,Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.

14. Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga;Na wazao wake hawatashiba chakula.

15. Hao watakaosalia kwake watazikwa katika kufa,Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.

16. Ajapokusanya fedha kama mavumbi,Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;

Ayu. 27