7. Adui yangu na awe kama huyo mwovu,Na mwenye kuondoka kinyume changu na awe kama asiye haki.
8. Kwani tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida,Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?
9. Je! Mungu atakisikia kilio chake,Taabu zitakapomfikilia?
10. Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi,Na kumlingana Mungu nyakati zote?
11. Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu;Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.
12. Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe;Mbona basi mmebatilika kabisa?