1. Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,
2. Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu;Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;
3. (Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu,Na roho ya Mungu i katika pua yangu;)
4. Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki,Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5. Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki;Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.