8. Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito;Na hilo wingu halipasuki chini yake.
9. Husitiri uso wa kiti chake cha enzi,Na kulitandaza wingu lake juu yake.
10. Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji,Hata hapo mwanga na giza vinapopakana.
11. Nguzo za mbingu zatetemeka,Na kustaajabu kwa kukemea kwake.
12. Huichafua bahari kwa uwezo wake,Na kumtema Rahabu kwa akili zake.
13. Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake;Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.
14. Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake;Na jinsi yalivyo madogo manong’ono tusikiayo katika habari zake!Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuelewa nazo?