25. Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai,Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi,Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
27. Nami nitamwona mimi nafsi yangu,Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine.Mtima wangu unazimia ndani yangu!
28. Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi!Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
29. Uogopeni upanga;Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu,Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.