Ayu. 19:25-29 Swahili Union Version (SUV)

25. Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai,Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.

26. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi,Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;

27. Nami nitamwona mimi nafsi yangu,Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine.Mtima wangu unazimia ndani yangu!

28. Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi!Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;

29. Uogopeni upanga;Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu,Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.

Ayu. 19