23. Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa!Laiti yangeandikwa kitabuni!
24. Yakachorwa katika mwamba milele,Kwa kalamu ya chuma na risasi.
25. Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai,Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi,Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
27. Nami nitamwona mimi nafsi yangu,Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine.Mtima wangu unazimia ndani yangu!