7. Lakini sasa amenichokesha;Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.
8. Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu;Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.
9. Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea;Amesaga-saga meno juu yangu;Mtesi wangu hunikazia macho makali.
10. Wamenifumbulia vinywa vyao;Wamenipiga shavuni kwa kunitukana;Hujikutanisha pamoja juu yangu.
11. Mungu amenitia kwa hao wapotovu,Na kunitupa mikononi mwao waovu.
12. Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja;Naam, amenishika shingo, na kuniponda;Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.