Ayu. 16:7-12 Swahili Union Version (SUV)

7. Lakini sasa amenichokesha;Jamii yangu yote umeifanya ukiwa.

8. Umenishika sana, ni ushahidi juu yangu;Na kukonda kwangu kwaniinukia, kwanishuhudia usoni pangu.

9. Amenirarua katika ghadhabu zake, na kunionea;Amesaga-saga meno juu yangu;Mtesi wangu hunikazia macho makali.

10. Wamenifumbulia vinywa vyao;Wamenipiga shavuni kwa kunitukana;Hujikutanisha pamoja juu yangu.

11. Mungu amenitia kwa hao wapotovu,Na kunitupa mikononi mwao waovu.

12. Nilikuwa katika raha, naye akanivunja-vunja;Naam, amenishika shingo, na kuniponda;Tena amenisimamisha niwe shabaha yake.

Ayu. 16