Ayu. 12:4-10 Swahili Union Version (SUV)

4. Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake,Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu;Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.

5. Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau mashaka;Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.

6. Hema za wapokonyi hufanikiwa,Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama;Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.

7. Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha;Na nyuni wa angani, nao watakuambia;

8. Au nena na nchi, nayo itakufundisha;Nao samaki wa baharini watakutangazia.

9. Katika hawa wote ni yupi asiyejua,Kwamba ni mkono wa BWANA uliofanya haya?

10. Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake,Na pumzi zao wanadamu wote.

Ayu. 12