17. Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani,Na Dani, mbona alikaa katika merikebu?Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari,Alikaa katika hori zake.
18. Zabuloni ndio watu waliohatirisha roho zao hata kufa;Nao Naftali mahali palipoinuka kondeni.
19. Wafalme walikuja wakafanya vita,Ndipo wafalme wa Kanaani walifanya vita.Katika Taanaki, karibu na maji ya Megido;Hawakupata faida yo yote ya fedha.
20. Walipigana kutoka mbinguni,Nyota katika miendo yao zilipigana na Sisera.
21. Mto ule wa Kishoni uliwachukua,Ule mto wa zamani, mto wa Kishoni.Ee roho yangu, endelea mbele kwa nguvu.