2 Sam. 23:21-32 Swahili Union Version (SUV)

21. huyo naye akamwua Mmisri, mtu mrefu; naye huyo Mmisri alikuwa na mkuki mkononi; lakini yeye alimshukia na gongo, akamnyakulia Mmisri mkuki mkononi mwake, akamwua kwa mkuki wake mwenyewe.

22. Hayo ndiyo aliyoyafanya Benaya, mwana wa Yehoyada, akawa na jina kati ya wale mashujaa watatu.

23. Alikuwa mwenye heshima kuliko wale thelathini, ila hakudiriki kuwamo katika wale watatu. Naye Daudi akamweka juu ya walinzi wake.

24. Asaheli, nduguye Yoabu, alikuwa mmojawapo wa wale thelathini; na Elhanani, mwana wa Dodo, wa Bethlehemu;

25. na Shama, Mharodi, na Elika, Mharodi;

26. na Helesi, Mpeloni, na Ira, mwana wa Ikeshi, Mtekoi;

27. na Abiezeri, Mwanathothi, na Sibekai, Mhushathi;

28. na Salmoni, Mwahohi, na Maharai, Mnetofathi;

29. na Heledi, mwana wa Baana, Mnetofathi, na Itai, mwana wa Ribai, wa Gibea wa wana wa Benyamini;

30. na Benaya, Mpirathoni, na Hurai, wa vijito vya Gaashi;

31. na Abieli, Mwarbathi, na Azmawethi, Mbarhumi;

32. na Eliaba, Mshaalboni, na wana wa Yasheni; na Yonathani,

2 Sam. 23