2 Nya. 11:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Lakini neno la BWANA likamjia Shemaya mtu wa Mungu, kusema,

3. Mwambie Rehoboamu mwana wa Sulemani, mfalme wa Yuda, uwaambie na Israeli wote waliomo Yuda na Benyamini, ukisema,

4. BWANA asema hivi, Hamtapanda wala kupigana na ndugu zenu; rudini kila mtu nyumbani kwake; kwa kuwa jambo hili limetoka kwangu. Basi, wakayasikiliza maneno ya BWANA, wakarudi katika kumwendea Yeroboamu.

5. Naye Rehoboamu akakaa Yerusalemu, akajenga miji yenye ngome katika Yuda.

6. Akajenga na Bethlehemu, na Etamu, na Tekoa,

7. na Bethsuri, na Soko, na Adulamu,

2 Nya. 11