16. Nasema tena, mtu asidhani ya kuwa mimi ni mpumbavu; lakini mjaponidhania hivi, mnikubali kama mpumbavu; ili mimi nami nipate kujisifu ngaa kidogo.
17. Ninenalo silineni agizo la Bwana, bali kama kwa upumbavu, katika ujasiri huu wa kujisifu.
18. Kwa sababu wengi wanajisifu kwa jinsi ya mwili, mimi nami nitajisifu.
19. Ninyi, kwa kuwa mna akili, mnachukuliana na wajinga kwa furaha.
20. Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.