2 Fal. 2:19-22 Swahili Union Version (SUV)

19. Watu wa mjini wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza.

20. Akasema, Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea.

21. Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, BWANA asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza.

22. Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.

2 Fal. 2