1 Sam. 20:37-40 Swahili Union Version (SUV)

37. Na mtoto alipofika penye ule mshale alioupiga Yonathani, Yonathani akampigia mtoto kelele, akasema, Je! Mshale si huko mbele yako?

38. Yonathani akampigia mtoto kelele, Haya! Hima! Usikawie. Mtoto wa Yonathani akaikusanya mishale, akaenda kwa bwana wake.

39. Lakini yule mtoto hakujua lo lote. Yonathani na Daudi ndio walioijua habari yenyewe.

40. Naye Yonathani akampa mtoto silaha zake, akamwambia, Nenda, ukazichukue mjini.

1 Sam. 20