2. Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA;Kwa maana hakuna ye yote ila wewe,Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3. Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;Majivuno yasitoke vinywani mwenu;Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.
4. Pinde zao mashujaa zimevunjika,Na hao waliojikwaa wamefungiwa nguvu.
5. Walioshiba wamejikodisha ili kupata chakula,Na hao waliokuwa na njaa wamepata raha.Naam, huyo aliyekua tasa amezaa watoto saba,Na yeye aliye na wana wengi amedhoofika.
6. BWANA huua, naye hufanya kuwa hai;Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.
7. BWANA hufukarisha mtu, naye hutajirisha;Hushusha chini, tena huinua juu.
8. Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,Humpandisha mhitaji kutoka jaani,Ili awaketishe pamoja na wakuu,Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu;Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA,Naye ameuweka ulimwengu juu yake.