1 Nya. 6:64-81 Swahili Union Version (SUV)

64. Na wana wa Israeli waliwapa Walawi miji hiyo pamoja na viunga vyake.

65. Tena wakawapa kwa kura miji hiyo iliyotajwa majina yake, katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, na katika kabila ya wana wa Benyamini.

66. Na jamaa nyingine za wana wa Kohathi walikuwa na miji ya mipakani mwao katika kabila ya Efraimu.

67. Basi wakapewa miji ya kukimbilia, yaani, Shekemu pamoja na viunga vyake katika nchi ya milima milima ya Efraimu; na Gezeri pamoja na viunga vyake;

68. na Yokmeamu pamoja na viunga vyake, na Beth-horoni pamoja na viunga vyake;

69. na Aiyaloni pamoja na viunga vyake, na Gath-rimoni pamoja na viunga vyake;

70. na katika nusu-kabila ya Manase; Taanaki pamoja na viunga vyake, na Ibleamu pamoja na viunga vyake; kwa mabaki ya jamaa ya wana wa Kohathi.

71. Na wana wa Gershoni wakapewa, katika jamaa ya nusu-kabila ya Manase; Golani katika Bashani pamoja na viunga vyake, na Ashtarothi pamoja na viunga vyake;

72. na katika kabila ya Isakari; Kishioni pamoja na viunga vyake, na Daberathi pamoja na viunga vyake;

73. na Remethi pamoja na viunga vyake, na En-gaminu pamoja na viunga vyake;

74. na katika kabila ya Asheri; Mishali pamoja na viunga vyake, na Abdoni pamoja na viunga vyake;

75. na Helkathi pamoja na viunga vyake, na Rehobu pamoja na viunga vyake;

76. na katika kabila ya Naftali; Kedeshi katika Galilaya pamoja na viunga vyake, na Hamothi pamoja na viunga vyake, na Kiriathaimu pamoja na viunga vyake.

77. Nao mabaki ya Walawi, wana wa Merari, wakapewa, katika kabila ya Zabuloni; Rimona pamoja na viunga vyake, na Tabori pamoja na viunga vyake;

78. na ng’ambo ya mto wa Yordani huko Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, katika kabila ya Reubeni; Bezeri katika nyika pamoja na viunga vyake, na Yahasa pamoja na viunga vyake,

79. na Kedemothi pamoja na viunga vyake, na Mefaathi pamoja na viunga vyake;

80. na katika kabila ya Gadi; Ramothi katika Gileadi pamoja na viunga vyake, na Mahanaimu pamoja na viunga vyake;

81. na Heshboni pamoja na viunga vyake, na Yazeri pamoja na viunga vyake.

1 Nya. 6