1 Nya. 6:53-61 Swahili Union Version (SUV)

53. na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.

54. Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;

55. wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;

56. bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.

57. Na wana wa Haruni wakapewa miji ile ya kukimbilia, nayo ni Hebroni, tena Libna pamoja na viunga vyake, na Yatiri, na Eshtemoa pamoja na viunga vyake;

58. na Holoni pamoja na viunga vyake, na Debiri pamoja na viunga vyake;

59. na Ashani pamoja na viunga vyake, na Beth-shemeshi pamoja na viunga vyake;

60. tena katika kabila ya Benyamini; Geba pamoja na viunga vyake, na Alemethi pamoja na viunga vyake, na Anathothi pamoja na viunga vyake. Miji yao yote katika jamaa zao ilikuwa miji kumi na mitatu.

61. Nao waliobaki wa wana wa Kohathi walipewa kwa kura miji kumi, katika jamaa ya kabila hiyo, yaani, nusu-kabila, nusu ya Manase.

1 Nya. 6