5. Naye Ashuri, babaye Tekoa, alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.
6. Naye Naara akamzalia Ahuzamu, na Heferi, na Temeni, na Ahashtari. Hao ndio wana wa Naara.
7. Na wana wa Hela walikuwa Serethi, na Ishari, na Ethnani.
8. Na Hakosi akawazaa Anubu, na Sobeba, na jamaa za Aharheli, mwana wa Harumu.
9. Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze; na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa huzuni.