1 Nya. 24:6-20 Swahili Union Version (SUV)

6. Naye Shemaya, mwana wa Nethaneli, mwandishi, aliyekuwa wa Walawi, akawaandika mbele ya mfalme, na mbele ya wakuu, na Sadoki kuhani, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari, na wakuu wa mbari za baba za makuhani, na za Walawi; ikatwaliwa ya Eleazari mbari moja ya baba, na moja ikatwaliwa ya Ithamari.

7. Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya;

8. ya tatu Harimu, ya nne Seorimu;

9. ya tano Malkia, ya sita Miyamini;

10. ya saba Hakosi, ya nane Abia;

11. ya kenda Yeshua, ya kumi Shekania;

12. ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu;

13. ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu;

14. ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri;

15. ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi;

16. ya kumi na kenda Pethahia, ya ishirini Ezekieli;

17. ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli;

18. ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.

19. Huu ndio usimamizi wao katika huduma yao, waingie nyumbani mwa BWANA kwa kadiri ya agizo lao, kwa mkono wa Haruni baba yao, kama BWANA, Mungu wa Israeli, alivyomwamuru.

20. Na wa wana wa Lawi, waliosalia; wa wana wa Amramu, Shebueli; wa wana wa Shebueli, Yedeya.

1 Nya. 24