1 Nya. 16:9-14 Swahili Union Version (SUV)

9. Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi;Zitafakarini ajabu zake zote.

10. Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.

11. Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.

12. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;

13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.

1 Nya. 16