8. Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;Wajulisheni watu matendo yake.
9. Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi;Zitafakarini ajabu zake zote.
10. Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.
11. Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.