1 Nya. 16:7-18 Swahili Union Version (SUV)

7. Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru BWANA, kwa mkono wa Asafu na nduguze.

8. Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;Wajulisheni watu matendo yake.

9. Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi;Zitafakarini ajabu zake zote.

10. Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.

11. Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.

12. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;

13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.

15. Likumbukeni agano lake milele,Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.

16. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka;

17. Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri,Na Israeli liwe agano la milele.

18. Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa;

1 Nya. 16