7. Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru BWANA, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
8. Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;Wajulisheni watu matendo yake.
9. Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi;Zitafakarini ajabu zake zote.
10. Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.
11. Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.
12. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.
15. Likumbukeni agano lake milele,Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
16. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka;
17. Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri,Na Israeli liwe agano la milele.
18. Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa;