1 Nya. 16:30-35 Swahili Union Version (SUV)

30. Tetemekeni mbele zake, nchi yote.Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

31. Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie;Na waseme katika mataifa, BWANA ametamalaki;

32. Bahari na ivume na vyote viijazavyo;Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;

33. Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha,Mbele za BWANA,Kwa maana anakuja aihukumu nchi.

34. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

35. Nanyi mkaseme,Ee Mungu wa wokovu wetu, utuokoe,Utukusanye kwa kututoa katika mataifa,Tulishukuru jina lako takatifu,Tuzifanyie shangwe sifa zako.

1 Nya. 16