24. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.
25. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
26. Maana miungu yote ya watu si kitu;Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.
27. Heshima na adhama ziko mbele zake;Nguvu na furaha zipo mahali pake.
28. Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu.
29. Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Leteni sadaka, mje mbele zake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;
30. Tetemekeni mbele zake, nchi yote.Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;
31. Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie;Na waseme katika mataifa, BWANA ametamalaki;
32. Bahari na ivume na vyote viijazavyo;Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;
33. Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha,Mbele za BWANA,Kwa maana anakuja aihukumu nchi.
34. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
35. Nanyi mkaseme,Ee Mungu wa wokovu wetu, utuokoe,Utukusanye kwa kututoa katika mataifa,Tulishukuru jina lako takatifu,Tuzifanyie shangwe sifa zako.