22. Akisema, Msiwaguse masihi wangu,Wala msiwadhuru nabii zangu.
23. Mwimbieni BWANA, nchi yote;Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
24. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.
25. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
26. Maana miungu yote ya watu si kitu;Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.
27. Heshima na adhama ziko mbele zake;Nguvu na furaha zipo mahali pake.
28. Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu.
29. Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Leteni sadaka, mje mbele zake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;
30. Tetemekeni mbele zake, nchi yote.Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;
31. Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie;Na waseme katika mataifa, BWANA ametamalaki;
32. Bahari na ivume na vyote viijazavyo;Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;