1 Nya. 16:20-30 Swahili Union Version (SUV)

20. Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa,Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.

21. Hakumwacha mtu awaonee;Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;

22. Akisema, Msiwaguse masihi wangu,Wala msiwadhuru nabii zangu.

23. Mwimbieni BWANA, nchi yote;Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.

24. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.

25. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.

26. Maana miungu yote ya watu si kitu;Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.

27. Heshima na adhama ziko mbele zake;Nguvu na furaha zipo mahali pake.

28. Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu.

29. Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Leteni sadaka, mje mbele zake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;

30. Tetemekeni mbele zake, nchi yote.Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

1 Nya. 16