1 Nya. 16:13-25 Swahili Union Version (SUV)

13. Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake,Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.

15. Likumbukeni agano lake milele,Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.

16. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka;

17. Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri,Na Israeli liwe agano la milele.

18. Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa;

19. Mlipokuwa watu wawezao kuhesabiwa;Naam, watu wachache na wageni ndani yake.

20. Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa,Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.

21. Hakumwacha mtu awaonee;Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;

22. Akisema, Msiwaguse masihi wangu,Wala msiwadhuru nabii zangu.

23. Mwimbieni BWANA, nchi yote;Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.

24. Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.

25. Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.

1 Nya. 16